NAFDA

NAMFUA FLAG DEVELOPMENT ASSOCIATION.

Friday, August 14, 2015


RAIS KIKWETE AZINDUA HATI ZA AHADI YA UADILIFU KWA VIONGOZI
unnamedRais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini Hati za Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi, Watumishi wa Umma na Sekta binafsi akishuhudiwa na viongozi wa taasisi na sekta hizo leo Agosti 14, 2015 Ikulu jijini Dar es salaam.
…………………………………………………………………..
Na Lilian Lundo, MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete  amezipongeza sekta binafsi kwa kukubali kusaini hati  ya ahadi ya uadilifu  katika harakati za mapambano dhidi ya rushwa na utovu wa nidhamu.
 Rais alisema hayo katika wakati akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa hati hizo zinazojumuisha sekta ya Umma na  Binafsi katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Katika hafla hiyo,  Mhe. Rais alisaini hati tatu ambazo ni Hati ya ahadi ya uadilifu ya Viongozi wa Umma, hati ya ahadi ya uadilifu ya Utumishi wa Umma na hati ya uadilifu ya Sekta Binafsi.
“Ushiriki wa sekta binafsi katika hati hii utasaidia kuleta mabadiliko ya kuwa na mwenendo wa kimaadili ya mapambano dhidi ya rushwa” alisema Mhe. Kikwete.
Rais Kikwete alisema kuwa badala ya wananchi na sekta binafsi kulalamika pembeni ni vyema kuwasilisha malalamiko yao katika sehemu husika ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.
 Aidha, Rais aliongeza kuwa baadhi ya sekta binafsi  zimekuwa zikiombwa na kutoa rushwa  ili kupewa  upendeleo wa kupata  tenda serikalini, hivyo kwa kusaini hati   hiyo ya ahadi ya uadilifu kutaondoa mianya ya  upokeaji na utoaji rushwa katika sekta hiyo.
Hati ya ahadi ya uadilifu inakumbusha Makampuni, Viongozi na Watumishi wa Umma juu ya wajibu wao wa kuzingatia kanuni za maadili na mapambano dhidi ya rushwa nchini.
Wazo la kuwa na ahadi ya uadilifu liliibuliwa katika maabara ya Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ambapo ilionekanakuwa rushwa bado ni tatizo katika uendeshaji wa shughuli za Umma na Binafsi hususani utoaji huduma kwa umma na biashara.
SUGU, NATURE, PROFESSA J KUFANYA SHOO YA KUHAMASISHA MASHABIKI KUPIGA KURA OKTOBA 25, 2015
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Kala Jeremiah akiongea na waandishi wa habari ili kuwaelezea onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. Pembeni ni Joseph Haule “Professa J”, Juma Kassim “Sir Nature” pamoja na Msagasumu.
 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. 
 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Juma Kassim “Sir Nature” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.
Tanzania Oyeeeee! Tanzania Oyeeee! ndiyo wasanii hawa walivyokuwa wakitia msisitizo.
 Baadhi ya wasanii watakaowasha moto Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015.
Mwandishi wa habari wa Times Fm, akifanya mahojiano na Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J”.
Na Mwandishi Wetu.
Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya na baadhi ya nyota wa Bongo Movie watafanya onyesho la bure Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.
Wasanii hao wataongozwa na Mbunge wa Mbeya mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Mbilinyi “Sugu” na nyota wengine kama Juma Kassim “Sir Nature”, Joseph Haule “Professa J” na Kara Jeremiah.
Wengine ni watakaopanda jukwaani siku kuanzia saa 8.00 mchana ni Msaga Sumu, Baba Haji na waigizaji nyota wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper na Auntie Ezekiel.
Akizungumza jijini jana, Professa J alisema kuwa sababu kubwa ya kufanya onyesho hilo ni kutoa elimu kwa mashabiki wao kuhusiana na zoezi la upigaji kura kuchagua viongozi bora wan chi hii wataodumu kwa miaka mitano.
Professa alisema kuwa wanataka kutoa mwamko kwa mashabiki wao kushiriki kwa wingi katika zoezi hilo ili kutumia demokrasia yao kumchagua kiongozi wanayemtaka.
“Tumejiandaa vilivyo kutoa elimu, lengo ni kuwahamasisha mashabiki wetu kufanya kile wanachokiona kinafaa ili kutimiza malengo yao ya kikatiba,” alisema Professa J.
Alisema kuwa mbali ya Dar es Salaam, onyesho hilo pia litafanyika katika mikoa mengine mbalimbali.
Akizungumza katika mkutano huo, Nature aliwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi ili kupata elimu hiyo ambayo wasanii wameamua kuitoa.
“Hii siyo kampeni ya kisiasa, sisi ni wasanii tumeamua kujitolea kufanya kazi ambayo wasanii wengi duniani wameifanya, lazima tutumie kazi yetu kutoa elimu kwa mashabiki ili wajue wajibu wao katika mambo mbali mbali pamoja na uchaguzi mkuu,” alisema Nature.
JWTZ YAKANUSHA KUWANYANG'ANYA KADI ZA KUPIGIA KURA MAOFISA NA ASKARI WAKE
Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wakati akikanusha jeshi hilo kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na kiongozi mmoja wa chama cha siasa. Kulia ni Msaidizi wa Kanali Lubinga, Meja Joseph Masanja na kushoto ni Kapteni Swaleh Omari.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale

JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limekanusha kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na mmoja wa viongozi wa chama kimoja cha siasa na kutolewa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.


Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga alisema madai hayo siyo ya kweli na  kuwa jeshi hilo halijafanya hivyo na wala haliwezi kufanya hivyo.

"Wanajeshi hawaruhusiwi kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa na kuwa mwanajeshi haruhusiwi kuwa shabiki wa chama chochote cha kisiasa.
Lubinga alisema Jeshi la Wananchi Tanzania linafanya kazi zake kama 'professional state organ duniani na kuwa mwanajeshi anayekiuka huchukuliwa hatua za kinidhamu za kijeshi wala si za kiraia. Alisema Jeshi la Wananchi Tanzania limesikitishwa na kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi huyo.

"Wananchi na viongozi wa kisiasa mnaombwa mfanye kazi zenu za kisiasa na zisianzishwe hoja nje ya maeneo hayo ya kisiasa kwani lugha hizo za upotoshaji zinaweza kuleta hofu, ukakasi na wasiwasi kwa wananchi" alisema Kanali Lubinga.

Kanali Lubinga alisema jeshi hilo linaendelea na shughuli zake kama kawaida halipendi litolewe kauli za upotoshaji, kusikoeleweka ufuatwe utaratibu wa kuuliza kupata majibu ya uhakika kwani wananchi wanaimani na jeshi lao.

Thursday, August 13, 2015


OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YATANGAZA MATOKEO YA TAKWIMU ZA PATO LA TAIFA
                     


X1
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam wakati akitangaza matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 ambayo yameonyesha kuwa thamani ya Pato la imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014.
X3
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke wakati akitangaza matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 ambayo yameonyesha kuwa thamani ya Pato la imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014.
Matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza yaani kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 yameonyesha kuwa thamani ya Pato la Taifa imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014.(VICTOR)

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke amesema takwimu hizo zimetayarishwa kwa kuzingatia marekebisho ya Takwimu za Pato la Taifa kwa bei za mwaka 2007.
“Pato la Taifa kwa bei za mwaka 2007 katika kipindi cha robo mwaka ya kwanza linaonyesha kuwa na jumla ya thamani ya shilingi trilioni 10.6 kwa mwaka 2015 ikilinganishwa na shilingi trilioni 9.9 katika kipindi kama hicho mwaka 2014”, amefafanua Oyuke.
Oyuke amesema kuwa, Pato hili la Taifa limeongezeka kwa kasi ya asilimia 6.5 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Aidha, Oyuke amesisitiza kuwa utayarishaji wa takwimu za Pato la Taifa hujumuisha shughuli zote za kiuchumi na hivyo hutumika katika kutathmini, kupanga mipango na kutayarisha sera za kiuchumi.
Baadhi ya shughuli hizo za uchumi ni kilimo na mifugo ambazo zilikua kwa kasi ya asilimia 2.6 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 3.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Uvuvi ziliongezeka kwa asilimia 0.9 kwa robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na asilimia 2.3 kipindi kama hicho mwaka 2014. Ukuaji huu ulitokana na jitihada za Serikali kuwasaidia wakulima kwa kutoa ruzuku na maelekezo ya Ma-ofisa Ugani kwa wakulima kama vile kuchagua mbegu bora yaliyosaidia kuongeza uzalishaji.
Shughuli za Uchimbaji Madini, Mawe na Kokoto ziliongezeka kwa kasi ya asilimia 0.6 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 19.7 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Uzalishaji bidhaa Viwandani zilikua kwa kasi ya asilimia 5.7 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.2 kipindi kama hicho mwaka mwaka 2014. Kasi ya ukuaji ilitokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa za vyakula, vinywaji, tumbaku, nguo, simenti na bidhaa za kemikali na madawa.
Shughuli nyingine ni pamoja na Uzalishaji nishati ya umeme na maji ambazo zilikua kwa kasi ya asilimia 10.7 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 10.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2014. Kuongezeka kwa ukuaji wa nishati ya umeme kulitokana na kuongezeka kwa umeme uliozalishwa kutoka kwenye mitambo inayotumia, maji, mafuta na gesi asilia.
Shughuli za Fedha na Bima katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ziliongezeka kwa asilimia 9.1 ikilinganishwa na asilimia 11.2 kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Ujenzi (ambazo zinajumuisha ujenzi wa nyumba za makazi na zisizo za makazi; barabara na madaraja; na shughuli nyingine za uhandisi) katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ziliongezeka kwa asilimia 8.8 ikilinganishwa na asilimia 21.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu ina jukumu la kutayarisha na kusambaza takwimu rasmi nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za Pato la Taifa kwa robo Mwaka ambazo hupimwa kwa kuangalia thamani ya bidhaa na huduma zilizozalishwa nchini katika vipindi vya miezi mitatu mitatu ambavyo ni Januari – Machi, Aprili – Juni, Julai – Septemba na Oktoba – Desemba.

COMPUTER OPERATORS Job at Western Zone Tobacco Growers Cooperative Union Ltd


Western Zone Tobacco Growers Cooperative Union Ltd is vested with the duties of providing high quality services to all tobacco farmers within the Region. Currently the Union is wishing to recruit highly motivated and dynamic staffs to fill in the following positions

COMPUTER OPERATORS (2 POSTS)

Key responsibilities.
To enter Commands, using computer terminal and activate controls on computer and peripheral equipment to integrate and operate equipment.
Monitor the system for equipment failure or errors in performance.
Notify system Administrator/Senior Computer Operator operations which are processed.
Operate spreadsheet programs and other types of software to load and manipulate date and to produce reports.
Supplying varieties of forms to primary societies which are instrument of collecting data/information and to instore in the computer.
And perform other duties as assigned by Senior Computer Operator.

Age within
(30 - 45) years.
Salary
As per WETCU scale 6
Experience

 At least three years work - experience in a Reputable
organization.

Term of Services

A two years renewable contract in mutual agreement.
APPLICATION INSTRUCTIONS:

All applications and detailed CV showing at least two referees should be sent to;
GENERAL MANAGER,
WETCU LTD.,
P.O. BOX 64, TABORA.
Email: wetcultd@yahoo.com
Telephone: 026 - 260 5270

JE TRAFIKI ANARUHUSIWA KUKUNYANG”ANYA LESENI ?




Kumekuwepo na sintofahamu nyingi kwa madereva na watumiaji wengine wa vyombo vya usafiri. Sintofahamu hii imekuwa ikiletwa na baadhi ya mambo ambayo hayaeleweki sawasawa katika suala zima la usalama barabarani na sheria zake. Wadau wa barabarani wamekuwa wakilaumiana, madereva wakiwalaumu askari wa barabarani kwa uonevu huku askari wa barabarani wakiwalaumu madereva kwa ukorofi na ukosefu wa utii wa sheria bila shuruti. Lakini swali hapa ni kwanini iwepo mivutano na hali kuna sheria. Sheria inasemaje kwa kila jambo ambalo wadau hawa wanatofautiana?.
1.UBABE WA ASKARI WA BARABARANI.
Baadhi ya askari wa barabarani wamekuwa ni wababe sana. Wanahoji mambo ambayo si wajibu wao kuyahoji na hawataki dereva aulize lolote kuhusu kuhoji kwao mambo hayo. Wanataka kila wanachosema dereva atii hata kama anaona hakipo kwa mujibu wa sheria. Matokeo yake mtu anaandikiwa faini za makosa mengi ilimradi tu kumkomoa. Askari wengine wamefikia hatua ya kuwapiga madereva vibao. Binafsi nimewahi kushuhudia askari wa usalama barabarani akimnasa kibao dereva wa daladala. Ni ubabe uliovuka mipaka na hakika ni uvunjaji wa sheria uliopitiliza.


2. JE TRAFIKI ANARUHUSIWA KUMNYANGANYA DEREVA LESENI.
Masuala ya usalama barabarani yanaainishwa ndani ya Sheria ya Usalama barabarani ( The Road Traffic Act) ambayo ndio hueleza wajibu na haki za kila mdau na mtumiaji wa barabara. Katika sheria hii hakuna pahala pameandikwa kuwa trafiki achukue leseni ya dereva kwa kuwa dereva ametenda kosa fulani. Maana fupi ya hili ni kuwa trafiki haruhusiwi kuchukua leseni ya dereva. Anachoweza kufanya trafiki ni kile kilichoainishwa na kifungu cha 17 cha sheria hiyo ya usalama barabarani. Kifungu hicho kinampa trafiki mamlaka ya kukagua na kujiridhisha na uhalali wa leseni ya dereva. Hakisemi aichukue. Kinasema aikague basi. Kukagua na kuchukua ni mambo mawili tofauti.
Kama hivyo ndivyo basi yafaa kueleweka kuwa kitendo cha askari kumsimamisha dereva na kisha kumpokonya leseni yake ni kinyume cha sheria.
Dereva anao wajibu wa kulinda haki hii kwa kulikataa hili na kuhakikisha trafiki hamfanyii kitendo hiki. Kumbuka kuwa wakati askari wa barabarani akitekeleza wajibu wake wa kisheria na wewe dereva unayo haki ya kutetea haki zako za kisheria. Hakuna aliye juu ya mwingine kwani anatekeleza wajibu nawe unalinda haki.
3. SAID MWEMA AKATAZA KUNYANGANYWA LESENI.
Mkuu wa jeshi la polisi mstaafu ndugu Saidi Mwema aliwahi kuandika kukemea hatua ya madereva kunyanganywa leseni. Katika kijarida alichokiita UMESIMAMISHWA NA POLISI UKIWA UNAENDESHA ?, ZIJUE HAKI NA WAJIBU WAKO, ndugu mwema ameandika akisema kuwa ofisa wa polisi hana haki ya kuchukua leseni ya dereva.
4. HAIRUHUSIWI KUBANDUA BIMA/ AU KIBANDIKO( STICKERS) KINGINE CHOCHOTE.
Wakati mwingine askari wa barabarani huamua kubandua bima au vibandiko vingine ( stickers) kwa lengo la kumfanya dereva amfuate au malengo mengine yoyote. Hili nalo ni kosa kwakuwa haliainishwi popote katika sheria. Jambo ambalo halikuruhusiwa na sheria kulitenda kwake ni kosa. Ieleweke kuwa askari wa barabarani haruhusiwi kubandua stika yoyote katika gari lako wala kuichukua.
5. UKIONEWA NA ASKARI WA BARABARANI CHUKUA HATUA HIZI.
Ili uweze kumchukulia hatua vizuri askari ni vema ukijua jina lake, cheo chake, na kituo anachotokea. Katika kuyajua haya ni lazima watu wajue kuwa ni haki yako kumuuliza askari taarifa hizi. Sio dhambi wala kosa ila ni haki kumuuliza askari taarifa hizi. Na kwa askari ni wajibu kukueleza taarifa hizi. Haijalishi mmeshatofautiana wala nini isipokuwa ni wajibu akupe taarifa hizi. Lakini ushauri ni kuwa ni vema zaidi askari anapokusimamisha tu kabla ya kujadili lolote kumuuliza au kumuomba ajitambulishe ili hata mkishatofautiana mbeleni iwe rahisi kwako kuchukua hatua.
Kiutaratibu inatakiwa askari ajitambulishe kwako bila wewe kumuuliza na kabla ya kuzungumza lolote lakini kwakuwa hawafanyi hivyo ndio maana wewe unalazimika kumuuliza. Baada ya kupata taarifa hizo peleka malalamiko yako kwa mkuu wa kituo anachotokea halafu fuatilia. Atachukuliwa hatua wala huna haja ya kulihofi hilo. Jeshi la polisi ni sehemu ambako nidhamu inazingatiwa kuliko pahali pengine popote hivyo unapomripoti askari ni lazima ashughulikiwe.
Kwa taarifa yako askari wanaogopa sana kuripotiwa kwa wakubwa zao kuliko watumishi wengine wowote wa umma unaowajua, hili nakupa. Na askari yoyote mwenye kujitambua akijua unalenga kumripoti ni lazima akubali myamalize. Basi usiishie kulalamika kwani kulalamika hakusaidii chukua hatua ili iwe funzo kwa wengine kesho na mbeleni.
MWANDISHI WA MAKALA HAYA NI MWANASHERIA NA MSHAURI WA SHERIA KUPITIA GAZETI LA SERIKALI LA HABARI LEO KILA JUMANNE , GAZETI JAMHURI KILA JUMANNE NA GAZETI NIPASHE KILA JUMATANO. 0784482959, 0714047241 bashiryakub@ymail.com

Monday, August 10, 2015

Rais Kikwete Atua mjini Dodoma Leo Kuendesha Vikao vya Chama cha Mapinduzi


Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Adam Kimbisa muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma.
  
Alhaj Kimbisa amekanusha uvumi uliosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa ameihama CCM. Kushoto ni Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na KAtibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahmana Kinana baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma.